}

YANGA YAJIFUA KUPINDUA MATOKEO KESHO

Yanga inaendelea na maandalizi yake ikiwa ugenini kwa ajili ya mchezo wao wa marudiano wa klabu bingwa Afrika dhidi ya Township Rollers ya Botswana utakaochezwa siku ya Jumamosi machi 17, 2018.

Mjumbe wa kamati ya utendaji na Katibu wa Kamati ya Mashindano Yanga Samuel Lukumay amesema kambi inaendelea vizuri kila kitu kipo sawa na wachezaji wote waliosafiri na timu wako salama kwa ajili ya mchezo wa Jumamosi.

“Maandalizi yanaendelea vizuri hatukupata shida yoyote tangu tunakuja hadi tumefika, tulitembelewa na balozi wa Tanzania nchini Afrika kusini ambaye ndio anasimamia pia Botswana akapata muda wa kuzungumza na vijana na kuwatia hamasa na kuwaambia katika mpira kilakitu kinawezekana kwa hiyo tunaweza kugeuza matokeo.”

“Hakuna majeruhi yoyote kiujumla kambi inaendelea vizuri bila tatizo lolote”

Mchezo wa awali uliozikutanisha yanga na Township Rollers kwenye uwanja wa Taifa, yanga ilipoteza kwa kufungwa 2-1 hivyo inahitaji kushinda kuanzia 2-0 ili kukata tiketi ya moja kwa moja kufuzu hatua ya makundi ya vilabu bingwa Afrika.

No comments

Haki zimehifadhiwa. Copyright, kituochahabari.com ©2016. Blog designed by Geofrey Donatus Jacka.. Powered by Blogger.