WAZIRI MPINA AITAKA KAMPUNI YA GAME TRACKING SAFARIS (TGTS) KUONDOKA KWENYE RANCHI YA UVINZA KABLA YA JANUARI 2018
Waziri wa Mifugo na uvuvi Mh.Luaga Mpina (Katikati) akizungumza jambo alipotembelea Ranchi ya mifugo ya Uvinza. |
Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mh. Luhaga Mpina ameutaka uongozi wa Kampuni ya Game Tracking Safaris(TGTS) kuangalia na kupitia nyaraka walizonazo ili kuona uhalali wa umiliki wa eneo la hekta 20000 kwenye vitalu tisa vilivyomo kwenye Ranchi ya Uvinza inayomilikiwa na Kampuni ya Ranchi za za Mifugo za Taifa (NARCO)kabla ya Selikali kuwatoa kwa nguvu ifikapo tarehe 1/1/2018.
Waziri Mpina amemuagiza Meneja Mkuu wa NARCO, Profesa Philemoni Wambura kuwaandikia barua ya kuwaondoa wawekezaji wote katika Ranchi hiyo ambao hawajaendeleza kwa zaidi ya asilimia 40 na kwamba wawekezaji ambao wamewekeza kwa zaidi ya asilimia arobaini wanatakiwa kukamilisha malipo yote kabla ya Januari mosi mwakani.
Awali, Meneja wa (TGTS) Audax Kalulama akizungumza kwa simu na Waziri Mpina kutoka Arusha amesema kwamba eneo hilo wanamiliki kihalali na kuomba muda ili wawasiliane na Wizara ya Mifugo kuonyesha taarifa za umiliki wa eneo hilo.
No comments