UPASUAJ WA KUREJESHA VIUNGO WAENDELEA AGAKHAN.
Hospitali ya Aga Kan kwa kushilikiana na Taasisi ya women for women na Hospitali ya Taifa Muhimbili leo wameendelea kufanya upasuaji wa kurudisha viungo vilivyotolewa katika mwili wa binadamu kutokana na ugonjwa wa saratani ikiwemo Matiti.
Akizungumza jijini Dar es
salam Daktari bingwa wa upasuaji kutoka Hospitali ya Aga Kan Aidan Njau amesema
kwa Tanzania ni mara ya kwanza kufanyika kwa upasuaji wa kumuwekea mwanamke
titi ambapo tayari wanawake wawili wamejitokeza kufanyiwa upasuaji huo.
Naye Daktari bingwa wa
upasuaji kutoka hospitali ya Taifa
Muhimbili Edwin Mrema amesema zoezi hilo ni mwendelezo wa kampeni ya kuwasaidia
kinamama na watoto ambao waliondolewa viongo vyao kwa kuungua na moto au kuugua saratani kurejea katika hali yao ya
kawaida.
No comments