Mkuu wa mkoa Geita aipongeza Halmashauri.
Mkuu wa Mkoa
wa Geita Mhandisi Robert Lughumbi ameipongeza Halmashauri ya Mji wa Geita kwa
kusimamia vizuri fedha za ujenzi wa vyumba vya madarasa vilivyo chini ya mpango
wa lipa kwa matokeo shule ya msingi Nguzo mbili.
Akizungumza
wakati wa ziara yake katika shule hiyo Mheshimiwa Robert Gabriel alisema kuwa
ameridhishwa na kiasi cha fedha kilichotumika katika ujenzi wa madarasa kwa
ubora wa hali ya juu katika shule hiyo.
" Inashangaza sana kuona maeneo mengine
wanatumia fedha zote kiasi cha shilingi 20 milioni katika ujenzi wa darasa moja
lakini kuna mapungufu mengi hivyo lazima kuwe na nidhamu ya matumizi ya fedha
katika miradi ya Serikali"Alisema Lughumbi.
Akiwa
shuleni hapo Mkuu wa Mkoa ameagiza wakurugenzi kuunda na kutumia vikundi vya
ujenzi vilivyo katika maeneo ya utekelezaji wa miradi ya ujenzi wa madarasa pia
kuishirikisha jamii ili kupunguza gharama kwa serikali na hatimaye fedha
zinazobaki ziwezekufanya mambo mengine katika huduma za jamii.
No comments