}

ANSAF YAISHAURI SERIKALI KUONGEZA MAAFISA UGANI.


Serikali imeshauriwa kuwaongeza Maafisa Ugani kwenye Halmashauri mbali mbali nchini ili kuweza kumsaidia  Mkulima  aweze kufanya Kilimo kwa Ufanisi .

Ushauri huo umetolewa leo Jijini Dar es Salaam na Mkurugenzi wa Mtendaji wa Jukwaa la wadau wa Kilimo (ANSAF),Audax Rukonge  wakati wa Mkutano uliowashirikisha wadau mbali mbali wa Kilimo AMBAPO amesema  kumtumia Afisa Mgani mmoja katika Kijiji kimoja  hakuna tija  wala  msaada wowote  kwa mkulima.

Aidha  amesema kuwa  kutokana na hali ilivyo ya uchache wa Maafisa Ugani kuna haja ya sekta binafsi kuwekeza kwenye utoaji wa Huduma ya  Ugani kwa Wakulima  ili iwe rahisi kwa Mkulima kusaidika.

Naye  Mhadhiri kutoka Chuo Kikuu cha Kilimo cha Sokine (SUA) Dk Sizya Lugeye, ameitaka  serikali Kuhakikisha wanawaongezea nguvu maafisa Ugani waliopo ikiwemo kuwapata fedha pamoja vitendea kazi ili waweze kufanya kazi kwa ufanizi zaidi katika kuwahudumia wakulima ili kukuza secta ya  kilimo nchini


No comments

Haki zimehifadhiwa. Copyright, kituochahabari.com ©2016. Blog designed by Geofrey Donatus Jacka.. Powered by Blogger.