}

KAMUSOKO, NGOMA NA TAMBE WAKO FIT KUIVAA SIMBA JUMAMOSI

KIUNGO Thabani Kamusoko na washambuliaji, Mzimbabwe mwenzake, Donald Ngoma na Mrundi Amissi Tambwe wanatarajiwa kuingia kambini leo usiku kuungana na wachezaji wenzao wa Yanga, kujiandaa na mchezo dhidi ya mahasimu wao wa jadi, Simba.

Nyasi bandia za Uwanja wa Uhuru mjini Dar es Salaam zinatarajiwa kutimbika kwa mchezo wa watani wa jadi wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara Jumamosi kuanzia Saa 10:00 jioni.

Na wakati kikosi cha Yanga kikiwa njiani kurejea Dar es Salaam kutoka Shinyanga ambako Jumapili walishinda 4-0 katika mchezo mwingine wa Ligi Kuu dhidi ya wenyeji, Stand United, Kamusoko, Ngoma na Tambwe waliokuwa majeruhi wanatarajiwa kuungana na wenzao leo.

No comments

Haki zimehifadhiwa. Copyright, kituochahabari.com ©2016. Blog designed by Geofrey Donatus Jacka.. Powered by Blogger.