}

SIMBA KUMPELEKA NIYONZIMA INDIA KUFANYIWA UPASUAJI

Kiungo wa Simba Haruna Niyonzima anatarajia kwenda nchini India kufanyiwa upasuaji mdogo kwenye mguu unaomsumbua na kumfanya asionekane uwanjani siku za karibuni kutokana na kuuguza majeraha.
Afisa habari wa Simba Haji Manara wakati akizungumza na waandishi wa habari amesema, Niyonzima ataondoka nchini ndani ya siku mbili hizi kuelekea India kwa ajili ya matibabu.
“Haruna Niyonzima anatarajia kusafiri ndani ya siku hizi mbili kwenda India kwa ajili ya kufanyiwa upasuaji mdogo kwenye mguu kutokana na maumivu yanayoendelea kumsumbua, haitachukua zaidi ya wiki mbili atakuwa amerejea uwanjani kwa sababu ni upasuaji mdogo tu”-Haji Manara, afisa habari Simba.
Niyonzima ambaye alisajiwa na Simba baada ya kumaliza mkataba wake na Yanga hajaonekana uwanjani katika mechi kadhaa na imekua ikielezwa kwamba ni kutokana na majeraha.
Kuhusu wachezaji wengine waliokuwa wanasumbuliwa na majeraha ya mufa mrefu (Said Mohamed ‘Nduda’ na Salim Mbonde) Manara amesema nyota hao wapo tayari kuendelea na mazoezi ya pamoja na timu nzima.
“Wachezaji wengine wa Simba ambao walikuwa na majeraha wameanza kurejea kwenye mazoezi ya pamoja na timu. Said Mohamed ‘Nduda’ ameshaanza mazoezi lakini Salim Mbonde anatarajia kujiunga mazoezini wakati wowote kwa sababu ameshamaliza program ya gym na beach.”

No comments

Haki zimehifadhiwa. Copyright, kituochahabari.com ©2016. Blog designed by Geofrey Donatus Jacka.. Powered by Blogger.