}

KILIMANJARO STARS KUKICHAFUA NA LIBYA KESHO MICHUANO YA CECAFA.

Kilimanjaro Stars - Timu ya Taifa ya Tanzania Bara kesho Jumapili Desemba 3, 2017 itacheza na Libya katika mchezo wa pili wa michuano ya kuwania Kombe la CECAFA - linaloandaliwa na Baraza la Soka la Afrika Mashariki.

Mchezo huo utakaofanyika Uwanja wa Machakos, utaanza saa 10:00 jioni (1600h) mara baada ya mchezo wa kwanza kati ya Kenya ‘Harambee Stars’ na Amavubi ya Rwanda utakaoanza saa 8.00 alasiri (1400h) utakaofanyika Uwanja wa Kakamega.

Michezo hiyo kama ilivyo kwa michezo mingine katika michuano hiyo itakuwa mubashara kutoka Kenya kwenye vituo mbalimbali vya televisheni ikiwamo Azam TV ya Tanzania.

Kilimanjaro Stars tayari wana shime kutoka kwa Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dk. Harrison Mwakyembe, Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Wallace Karia na Kocha Mkuu wa timu hiyo, Ammy Ninje.

No comments

Haki zimehifadhiwa. Copyright, kituochahabari.com ©2016. Blog designed by Geofrey Donatus Jacka.. Powered by Blogger.