WANAHABARI WATAKIWA KURIPOTI MIRADI NA PROGRAMU ZA SADC.
Na.Anaseli Stanley Macha.
Waratibu wa vyombo vya Habari wa nchi Wanachama wa Jumuiya ya Maendeleo ya Kusini mwa Afrika (SADC) wametakiwa kuhamasisha vyombo vya habari katika nchi wanachama kuripoti habari za miradi na progamu zinazotekelezwa na umoja huo kwa manufaa ya wananchi wa nchi wanachama.
Akizungumza katika washa ya ufunguzi Mkuu wa mawasiliano wa Jumuiya hiyo Bi. Barbara Lopi amesema lengo ni kuwajengea uwezo waratibu hao kuhamasisha vyombo vya habari kutangaza umuhimu wa wananchi kutumia fursa zilizopo katika nchi wanachama kuchochea maendeleo na Ustawi wa umoja huo.
Bi. Lopi ameongeza kuwa warsha hiyo itawajengea uwezo waratibu wa vyombo vya habari wa nchi Wanachama wa namna bora yakushirikiana na vyombo vya habari katika kutangaza miradi inayochochea ukuaji wa uchumi kwa nchi wanachama inayotekelezwa na SADC.
Baadhi ya mada zitakazowasilishwa katika warsha hiyo ni pamoja na Muundo wa Jumuiya hiyo,Umuhimu na Majukumu ya Waratibu wa Vyombo vya Habari kwa kila nchi.
Waratibu wa vyombo vya Habari wa nchi Wanachama wa Jumuiya ya Maendeleo ya Kusini mwa Afrika (SADC) wametakiwa kuhamasisha vyombo vya habari katika nchi wanachama kuripoti habari za miradi na progamu zinazotekelezwa na umoja huo kwa manufaa ya wananchi wa nchi wanachama.
Akizungumza katika washa ya ufunguzi Mkuu wa mawasiliano wa Jumuiya hiyo Bi. Barbara Lopi amesema lengo ni kuwajengea uwezo waratibu hao kuhamasisha vyombo vya habari kutangaza umuhimu wa wananchi kutumia fursa zilizopo katika nchi wanachama kuchochea maendeleo na Ustawi wa umoja huo.
Bi. Lopi ameongeza kuwa warsha hiyo itawajengea uwezo waratibu wa vyombo vya habari wa nchi Wanachama wa namna bora yakushirikiana na vyombo vya habari katika kutangaza miradi inayochochea ukuaji wa uchumi kwa nchi wanachama inayotekelezwa na SADC.
Baadhi ya mada zitakazowasilishwa katika warsha hiyo ni pamoja na Muundo wa Jumuiya hiyo,Umuhimu na Majukumu ya Waratibu wa Vyombo vya Habari kwa kila nchi.
No comments