}

Naibu waziri wa Afya maendeleo ya jamii jinsia wazee na watoto Mh. Faustine Ndungulile ameitaka mamlaka ya chakula na dawa TFDA kutekeleza majukumu yake kwa ufanisi mkubwa

Naibu waziri wa Afya maendeleo ya jamii jinsia wazee na watoto Mh. Faustine Ndungulile ameitaka mamlaka ya chakula na dawa TFDA kutekeleza majukumu yake kwa ufanisi mkubwa ili dawa zote zinazoingia nchini ziwe na ubora unaohitajika

Mh. Ndungulile amesema hayo jijini dar es salaam katika uzinduzi wa Cheti cha mfumo wa uhakiki ubora wa huduma cha kiwango cha kimataifa cha ISO ambapo amesema kuwa kupatika ka Cheti hicho ni wazi kuwa mchango wa mamlaka ya chakula na dawa TFDA ni mkubwa kwa taifa hivyo wanatakiwa kuongeza juhudi ili kukabiliana na changamoto zinazowakabili.


Kwa upande wake mkurugenzi mkuu wa TFDA Bw.Hiiti Sillo amesema tangu walipopata Cheti hicho wamefanya ukaguzi wa kila mwaka ili kubaini kama bado mfumo huo unakidhi matakwa ya kiwango cha kimataifa na kusisitiza kuwa mfumo huo umezidi kuimarika na kutoa huduma sahihi kwa watumiaji.

No comments

Haki zimehifadhiwa. Copyright, kituochahabari.com ©2016. Blog designed by Geofrey Donatus Jacka.. Powered by Blogger.