MALIASILI NA UTALII YASAINI MKATABA WA TSH. BILIONI 340.
Serekali kupitia wizara ya maliasili na utalii kwa kushirikiana na benki ya dunia imeandaa mradi wa kuendeleza utalii kwa vivutio vilivyoko ukanda wa kusini mwa Tanzania kwa kusainiana mkataba wa masharti nafuu wa sh. Bilioni 340
Akizungumza na waandishi wa jijini Dar es salaam katibu mkuu wizara ya fedha Dotto James amesemakuwa mradi huo utasaidia kuibua frusa za za kiuchumi kusini mwa Tanzania kwenye sekta ya utalii
Kwa upande wake katibu mkuu wizara ya maliasili na utalii Gaudence Millanzi amesemakuwa fedha hizo zitasaidia kuboresha vivutio vya utalii kutengeneza miundombinu ikiwemo barabara na viwanja vya ndege pamoja na kuhakikisha Jamii za karibu na hifadhi zinafaidika kiuchumi
No comments