}

ARSENAL YAFANYA USAJILI WA KUVUNJA REKODI YA DUNIA , LIVERPOOL IKIVUTA MKWANJA MREFU

 


Klabu ya soka ya Arsenal ya wanawake wamefanya usajili wa rekodi ya dunia kwa kumsajili mshambuliaji Raia wa Canada Olivia Smith kutoka klabu ya Liverpool kwa kitita cha Euro million 1.

Olivia Smith anakuwa mchezaji wa kwanza kwa wanawake kufikia rekodi kusajiliwa kwa gaharama kubwa duniani


Smith mwenye umri wa miaka 20 akiwa na klabu ya Liverpool amecheza michezo 20 ya ligi kuu ya wanawake England na kufunga magoli saba.



Uhamisho wa mchezaji huyo kwenda Arsenal unavunja rekodi ya mchezaji Naomi Girma aliyesajiliwa na Chelsea mwezi januari kwa kitita cha Euro laki 9.




No comments

Haki zimehifadhiwa. Copyright, kituochahabari.com ©2016. Blog designed by Geofrey Donatus Jacka.. Powered by Blogger.