}

Maneno ya Masa Ubwire wa Ruvu shooting kwa Simba SC baada yakuipiga Prison.


Baada ya kupata ushindi dhidi ya tanzania prisons,uongozi wa  klabu ya Ruvu Shooting umejinasibu kutoka na ushindi katika mchezo wao dhidi ya wkundu wa msimbazi simba, 

Akiandika kwanye mitandao ya kijamii msemaji wa klabu ya soka ya ruvu shooting Masu Bwire amesema wanataisambaratisha simba kwa silaha moja tu ya RUNGU.

 Mazoezi yetu jana kwa ajili ya maandalizi ya mchezo wetu Ruvu Shooting dhidi ya Simba yalienda vizuri kwani timu tuliyofanyia mazoezi hayo, Tanzania Prisons mbali na uwezo mkubwa iliyonao katika kucheza mpira, ilionekana kama mdoli mbele ya mafundi wa kabumbu, Ruvu Shooting!

“Maana ya hii ni kwamba, Alhamisi, Desemba 29, 2016 katika uwanja wa Uhuru itakuwa kazi moja tu, kuwafurusha Simba ya Dar es salaam ili ubora wetu uendelee kuonekana kwa Watanzania, wapenzi, washabiki na Wadau wa soka,” ameandika Masau.

“Katika mzunguko wa kwanza, tulipokutana na timu hiyo ya Msimbazi, tuliingia vitani kukabiliana na timu hiyo kwa fimbo ya mwanzi kutokana na namna tulivyoitazama kiuwezo , tukaonhi. hakuna haja ya kutumia silaha kubwa kumshambulia Simba aliyechoka kwa njaa, goigoi, asiye na nguvu, fimbo tu itamtosha!

“Bahati mbaya sana, fimbo ile ilitandika katika moja ya mifupa ya mnyama huyo aliyekuwa amekondeana kwa njaa! Si unajua, njaa inavyokondesha na kufanya mifupa yote ya mnyama ihesabike? Kwa Simba hali ilikuwa hivyo, hivyo, fimbo ile tuliyoitumia ilipotandika mifupa yake iliyojichomoza, ilivunjiika kabla ya vita hivyo,” anasisitiza Masau.

“Simba akatushambulia kwa kutujeruhi mara mbili baada ya kumpa jeraha moja lililosababisha fimbo tuliyokuwatukiitumia kuvunjika!

Safari hii, tumeongeza uimara wa silaha yetu katika kumuungamiza mnyama huyo! Bado hatuhitaji bunduki katika kupambana naye, RUNGU tu litatosha kabisa kumumaliza Simba wa Msimb!

Wengi wataona kama maneno na porojo, lakini niwaahakikishie kwamba, hatutanii, tuko serious na hili, tunapeleka maumivu Msimbazi kwa RUNGU lililoandaliwa maalumu kwa ajili hi. 

No comments

Haki zimehifadhiwa. Copyright, kituochahabari.com ©2016. Blog designed by Geofrey Donatus Jacka.. Powered by Blogger.