Hizi hapa sababu za Mbeya City kutotangaza Bunduki zake mpya.
Uongozi wa klabu ya Mbeya City umeweka bayana sababu za kutokutangazwa kwa majina ya wachezaji wapya na wanaoachwa kwenye kikosi cha Mbeya City fc ambao wanatarajiwa kuanza kutumika katika mzunguko wa pili wa ligi kuu tanzania bara
Meneja wa klabu ya mbeya city Geofrey Katepa amesema kwamba kutokana kocha Kinnah Phiri kushindwa kuwasili jijini mbeya siku ya jana ili aweze kutangaza majina hayo ndio sababu pekee ya kushindwa kutangaza kikosi chao.
aidha katepa amema kocha kinnah phiri amashindwa kuwasili kutokana na sababu mbalimbali za kifamilia ambapo sasa anatarajiwa kutua hapa nchini siku ya jumatatu asubuhi na mchana kutangaza majina ya wachezaji wataounda kikosi cha mbeya city katika mzunguko wa pili wa ligi kuu tanzania bara
uongozi mbeya city ulipanga kutangaza majina ya wachezaji wataoachwa na wachezaji wapya mnamo novemba 30 na kusogeza mbele mpka siku ya jumatatu ambapo kocha Phiri atawasili hapa nchini asuhuhi akitokea jijini Blantyre nchini Malawi na kutangaza kikosi chake wakati wa mchana.
No comments