}

AZAM YAULA TENA NMB



Klabu ya Azam FC imeendelea kuingia kwenye neema mpya baada ya kuingia tena mkataba mpya wa Benki ya wazalendo ya NMB.
NMB wanaonekana kufurahishwa na mambo yalivyokwenda katika mkataba wao wa kwanza na NMB baada ya kuonekana kuutendea haki mkataba wao wa awali wa benki hiyo hivyo imewaongezea mwingine wa mwaka mmoja ambao utawasaidia kupambana kuchukua Ubingwa wa Ligi Kuu Bara msimu huu.







Akizungumza wakati wa kusainishana mkataba huo Mkurungezi wa NMB, Imeko Bussemaker, alisema kwamba wameamua kuingia mkataba mpya na Azam FC.

Bosi huyo ameweka wazi namna ambavyo wamevutiwa na Azam FC na namna walivyoheshimu mkataba wao.

Wanaamini Azam itaongeza wigo mkubwa katika kuzalisha wachezaji wachanga hapa nchini ambao wataiinua hata timu ya taifa wanayoidhamini pia.

Naye, Mtendaji Mkuu wa Azam FC, Abdul Mohamed, yeye amewashukuru NMB kwa udhamini huo “Niwashukuru sana kwa hili lakini huku napenda niwaahidi kua siku chache zijazo nitarudi hapa tena kuwakabidhi Kombe la Ligi Kuu Bara.

"Kwani tunaamini hadi  mwisho wa msimu mambo yatanyooka maana farsafa yetu kwa sasa tunaendelea kupambana kimyakimya kama tunamfukuza mwizi,” alisema Abdul.







No comments

Haki zimehifadhiwa. Copyright, kituochahabari.com ©2016. Blog designed by Geofrey Donatus Jacka.. Powered by Blogger.