}

MPIRA MAZOEZI SIO KUROGA: WAZIRI MWAKYEMBE.



Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dk. Harrison Mwakyembe amewaambia wachezaji wa timu ya mpira wa miguu ya Tanzania Bara, ‘Kilimanjaro Stars’, kuwa Tanzania inahitaji ushindi katika michuano ya Kombe la Baraza la Soka la Afrika Mashariki (CECAFA).

Dk. Mwakyembe aliyesema hayo jana Novemba 29, usiku wakati wa hafla ya chakula cha jioni ambako alitumia baraza hilo kuwaaga vijana hao akiwataka wachezaji wa timu hiyo kwenda Kenya kujitahidi.

“Msidharau mechi,” amesema Dk. Mwakyembe huku akisisitiza: “Tunataka ushindi. Mnakwenda Kenya kwa niaba ya Watanzania. Najua mmejiandaa vizuri kwa mazoezi maana siku hizi huwezi kushinda kwa kumtegemea (kuroga). Siku hizi mazoezi ni basic component.

No comments

Haki zimehifadhiwa. Copyright, kituochahabari.com ©2016. Blog designed by Geofrey Donatus Jacka.. Powered by Blogger.