}

CANADA YAIPA TANZANIA DOZI MIL 23 ZA VITAMINI A.

Serikali ya Canada kupitia Shirika lake linaloshughulika na masuala ya lishe duniani la Nutrition International imetoa dozi milioni 23 za vitamini A yenye thamani ya shilingi bilioni 1.3  kwa Serikali ya Tanzania ili kuokoa  maisha  kwa kuimarisha  kinga ya mwili dhidi ya maradhi kwa watoto.
Kauli hiyo imetolewa leo na Mjumbe wa Bodi wa Shirika la Nutrition International, ambaye pia ni  Rais mstaafu wa Awamu ya Tano, dokta Jakaya Kikwete kwenye Kituo Cha Afya  Cha Makuburi akiwa na ujumbe wa Canada ulioongozwa na  Waziri wa Maendeleo ya Kimataifa Randeep Sarai. 

Katika Hotuba yake Mhe. Dkt. Kikwete ameipongeza Serikali ya Canada kwa kuendelea kuwa mshirika wa kweli katika kuisaidia Tanzania  katika eneo la Afya. 

Aidha, amefafanua kwamba  Serikali ya Canada imeendelea kuwa mfadhiri mkuu katika eneo hili kutokana na ukweli kuwa Serikali ya Tanzania ni Serikali makini inayoaminika na mataifa mbalimbali duniani. 

Kwa upande wake, Sarai amesema mataifa haya mawili ya Canada na Tanzania yamekuwa na mahusiano mazuri katika Sekta ya Afya ambapo amesisitiza kuwa nchi yake itaendelea kushirikiana na Tanzania. 

Awali Naibu Waziri wa TAMISEMI anayeshughulikia eneo la Afya, Festo Dugange ameishukuru Serikali ya Canada kwa mchango mkubwa kwenye eneo la afya hususan usajili wa watoto chini ya miaka mitano hapa nchini. 
Amesema, vituo vya kuandikishia watoto vimeongezeka kutoka 139  mwaka 2013 hadi 12,025  Julai 2025 hivyo kupunguza  umbali wa kutoka kituo kimoja  hadi kingine kuwa ndani ya kilomita  5–6 kutoka kilimita 80–140 mwaka 2013. 



No comments

Haki zimehifadhiwa. Copyright, kituochahabari.com ©2016. Blog designed by Geofrey Donatus Jacka.. Powered by Blogger.