MKUTANO MKUU TPS SACCOS KUANZA NOVEMBA 18, 2021 JIJINI DODOMA.
Na. Geofrey Jacka-Dodoma
Akizungumza katika Semina hiyo ya kuwajengea uwezo wawakilishi wa Mkutano huo, mtoa mada ambaye ni mtaalamu wa masuala ya vyama vya Ushirika Dkt. Uronu amesema kuwa, wajumbe na wanachama wa TPS SACCOS wanapaswa kushikamana na kujua malengo ya Chama hicho, ikiwa ni pamoja na kusoma kanuni zinazoongoza vyama vya Ushirika, ili kuifanya Sacco's hiyo kusonga mbele.
Aidha wawakilishi wa Mkutano huo wamepata nafasi ya kuchangia hoja mbalimbali ikiwemo kiasi cha uchangiaji, huku wakiutaka uongozi wa ngazi za juu wa TPS SACCOS kupita katika vituo nchi nzima, kwa lengo la kutoa elimu kwa wanachama, kitu walichodai kitakuwa msaada, kwani ufafanuzi utakao tolewa na viongozi hao utakuwa ni wa kina, ukilinganisha na ule unaotolewa na wawakilishi wanaopatikana katika vituo husika.
No comments