}

WADAU WA MAZINGIRA (JET ) WAKO TAYARI KUTEKELEZA DIRA YA MAENDELEO 2050

WADAU wa Mazingira Nchini wamesema wako tayari kutekeleza Dira ya Taifa ya Maendeleo ya mwaka 2050 katika kuhimiza uchumi wa buluu  ambapo ndani ya miaka mitatu katika eneo la Tanga na Pemba zaidi ya hekta 90  za mikoko zimerejeshwa kuimarisha uthabiti wa fukwe na kuboresha uchumi wa wananchi wa maeneo hayo.

Wadau hao ni Chama Cha Waandishi wa Habari za Mazingira Tanzania(JET) kwa kushirikiana na Taasisi ya kimataifa ya Masuala ya Hifadhi na Mazingira(IUCN) kupitia miradi ya Bahari Mali na kuwa stari  wa mbele  kuwahamasisha wananchi kufanya shughuli endelevu na rafiki lwa mazingira.
Hatua hiyo ni sehemu ya juhudi pana zinazoongozwa na jamii katika uhifadhi wa mazingira ya baharini katika eneo la Tanga–Pemba, ambazo tayari zimeleta manufaa makubwa ya kiikolojia na kiuchumi
 
Akizungumza na  katika mafunzo ya waandishi wa habari kuhusu  masuala ya uchumi wa buluu, yaliyoandaliwa  kwa ushirikiano na Chama Cha Waandishi wa Habari za Mazingira Tanzania(JET) na Taasisi ya kimataifa ya Masuala ya Hifadhi na Mazingira(IUCN) kupitia mradi ya Bahari Mali, Meneja wa Miradi ya Uhifadhi wa Bahari Joseph Olila alisema urejeshwaji huo ni sehemu ya mradi wa Bahari Mali unaolenga kutumia fursa ya uchumi wa buluu kwa njia jumuishi na endelevu kwa lengo la  kulinda bayoanuwai ya Pwani na baharini.

Pia, mradi huo unahusisha upandaji wa mikoko katika maeneo yaliyoharibiwa na kuwajengea uwezo wanajamii katika shughuli mbadala za kiuchumi kama vile ufugaji wa nyuki  sio kusaidia malengo ya mazingira tu bali na kuongeza  kipato kwa kaya husika.

Akizungumzia mradi huo alisema lengo ni  kusaidia shughuli za uchumi wa buluu katika eneo  la Tanga kwa wilaya ya Mkinga, Pangani  na Pemba kwa wilaya mbili ambazo Mkoani na Micheweni.

Alisema program hiyo imewawezesha wananchi  kujikwamua na umaskini na kufanya shughuli zao ambazo ni endelevu na rafiki kwa mazingira.

Kuhusiana na tafiti kwa kushirikiana na wadau wengine wamefanikiwa kuangalia eneo la asidi katika bahari hivyo mradi huo utawasaidia wanajamii kutambua fursa zitokanazo na bahari na kurejesha uoto wa asili.
Kwa upande wake, Mtafiti Mwandamizi Asasi ya Utafiti Uvuvi Tanzania (TAFIRI),Rushingisha George alisema wakiwa wanafanya tafiti wanatarajia matokeo ambayo yatumike kuboresha shughuli zote za uhifadhi.

No comments

Haki zimehifadhiwa. Copyright, kituochahabari.com ©2016. Blog designed by Geofrey Donatus Jacka.. Powered by Blogger.