}

Mafunzo yatolewa kwa wafanyakazi wa ndani.

Binagi Media Group
Utafiti uliofanywa na Shirika la hutetea haki za watoto wafanyakazi wanyumbani WOTESAWA Jijini Mwanza, unaonyesha kwamba watoto hao bado wanakumbana na aina mbalimbali za ukatili ikiwemo utumikishwaji.

Utafiti huo uliofanyika mwaka jana ulibaini kwamba asilimia 91.9 ya watoto wafanyakazi wa nyumbani katika Kata nne za Jiji hilo hawana mikataba ama makubaliano baina ya wazazi na waajiri wao, asilimia 5.4 wana mikataba huku asilimia 80 ikionyesha wapo wanaofanya kazi bila malipo huku wanaolipwa mshahara chini ya shilingi 20,000 wakiwa ni asilimia 20.

Utafiti huo ulifanyika katika Kata za Igogo ambapo watoto wafanyakazi wa nyumbani 43 walifikiwa, Mkuyuni 42, Nyamagana 32 pamoja na Butimba 37 na hivyo kufanya idadi ya watoto wafanyakazi wa nyumbani waliofikiwa kuwa 154, wavula wakiwa ni 16 na wasichana 138.


Hali hii inaongeza chachu kwa shirika la WOTESAWA kuwajengea uwezo watoto wafanyakazi wa nyumbani, waajiri wao pamoja na viongozi mbalimbali wakiwemo Madiwani, Watendaji, Wenyeviti wa Mitaa, Maafisa Ustawi wa Jamii, pamoja na maofisa wa dawati la jinsia kutoka jeshi la polisi kama anavyoeleza Mkurugenzi wa shirika hilo, Angel Benedicto.
Washiriki wa semina hi

No comments

Haki zimehifadhiwa. Copyright, kituochahabari.com ©2016. Blog designed by Geofrey Donatus Jacka.. Powered by Blogger.